Alhamisi, 19 Desemba 2013

Hii Ndio Siri ya LULU kuwa na shepu Bomba na ya Kuvutia..!!

SIRI ya muonekano mzuri wa msanii wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ imefichuka baada ya kubainika kuwa, amekuwa akifanya mazoezi kila siku kwa kwenda gym.



Lulu alianika siri hiyo hivi karibuni kupitia mtandao wa instargram kwa kutupia picha zikimuonesha akiwa kwenye tizi na baadae alipozi na kujifotoa picha ambazo zilimuonesha akiwa na umbo la kuvutia zaidi huku zikisindikizwa na maneno yasemayo; ‘ndiyo siri ya urembo’.
Hata hivyo, baadhi ya watu walioziona picha hizo walimpongeza kwa uamuzi wake huo huku ushauri pia ukitolewa kwa kila mmoja kujali afya yake kwa kufanya mazoezi pale muda unapopatikana

 Lulu akifanya mazoezi. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni