Alhamisi, 19 Desemba 2013

Hatimaye Mwenyekiti wa CCM jijini MWANZA aliyeuawa na Wananchi kwa Kupigwa mawe azikwa...!!

waombolezaji wakiingiza sanduku lenye mwili wa marehemu
Jeneza lenye mwili wa Clement Mabina likiwa mbele ya waombolezaji.
ALIYEWAHI kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mwanza na Diwani wa Kata ya Kisesa (CCM), Clement Mabina (56), amezikwa mchana huu shambani kwake Kanyamati, Kisesa mkoani Mwanza. Mazishi hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wasira, viongozi wa serikali, madhehebu ya dini, vyama vya siasa, wananchi na wakazi wa Kisesa ambao wameungana na ndugu, jamaa na marafiki kumsindikiza marehemu Mabina. Mazishi hayo yalitanguliwa na ibada iliyofanyika uwanja wa Ngomeni-Kisesa, Mwanza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni