Alhamisi, 22 Septemba 2016

Inasikitisha sana lakini itakufundisha


Huyu ni kijana anaitwa Nyamigawa Manoti.Si mkubwa sana bali ni kijana mdogo ila watu wazima waliomzidi umri walikuwa wanamwita mzee kwa sababu ya vujo zake kwenye pesa.Huyu ni kijana aliyezaliwa kwenye familia ya wafanyabiashara waliokuwa na fedha nyingi mno kutokana na kukwepa kulipa kodi.Miaka yoote ya biashara yao walikuwa wanapata faida haramu kwa sababu walikuwa na uwezo wa kuingiza mizigo mikubwa ya biashara bila ya wasiwasi wowote. Ndiyo si pale bandarini walikuwa wanajua wenyewe walichokuwa wanakifanya.Nyamigawa alikuwa ni kijana mwenye kugawa pesa kwa wingi kwa wanawake ,marafiki na watu mbalimbali ambao walikuwa wanamsifia na kumnyenyekea..Kila alipoona watu wamekaa wanacheza draft alikuwa anaona fahari kupita karibu yao na kusifiwa kuwa ni handsome mtanashati au kapendeza na kweli Nyamigawa alikuwa anafurahi mno kwa sifa zile na hakusita kutoa burungutu la pesa hata la shilingi laki nane na kuwapa wale woote waliokuwa wanamsifia ,ndiyo aliwapa usishangae si alikuwa na hela nyingi za biashara yao ambayo kampuni yao ilikuwa hailipi kodi ana wasi wasi gani ? Baba yake mzazi Nyamigawa Mzee Manoti Mazuta alikuwa na pesa nyingi kweli kweli, wakati mwengine alikuwa na pesa nyingi mno ambazo kuna wakati alikuwa anakwenda kuzigawa misikitini na kanisani,ndiyo aligawa sehemu mbalimbali kwenye mataasisi na sehemu nyengine. Mzee Manoti alikuwa anatoa pesa nyingi kwa watoto yatima,kwenye vikundi mbalimbali vya wanawake watoto na vijana,hakuishia hapo alikuwa anatoa pesa kwenye vyombo vya habari sana ili viwe vinamtangazia biashara yake..kwa kweli alifanikiwa naweza kusema maisha aliyapatia.Mzee huyo pamoja na mtoto wake Nyamigawa walipata kujulikana sana kwenye jamii na kila mtu aliwapenda kwa kweli alikuwa anaombewa dua nyingi na watu wa kila rika.Haaa huyu ndiyo mzee Manoti na mwanaye Nayamigawa..MIAKA MIWILI BAADAE Tanzania ikawa inafanya kampeni za uchaguzi mkuu watu wengi walikuwa wanashabikia vyama walivyovipenda hapa nchi iliingia kwenye heka heka za nguvu vyama vya upinzani vikaunda umoja wao na kuupa jina UKAWA vikawa vinashindana na chama tawala ambacho ni CCM  Mzee Manoti kwa kuwa ni mfanyabiashara akaona na yeye atumie fursa ya kujinufaisha kupitia uchaguzi huu mkubwa wa madiwani wabunge na ma rais akaenda kwenye chama tawala ili akipe fedha nyingi ziwasaidie kwenye kampeni Bahati nzuri mgombea wa chama hiko John Pombe Joseph Magufuli akazikataa zile pesa,ndiyo aliamua kuzikataa kwa sababu alishaona mbali,alishaona na kujua lengo la tajiri huyu alijua kuwa anataka kuficha dhambi zake kwenye mgongo wa kusaidia chama na ni kweli hasa hiyo ndiyo ilikuwa nia ya tajiri Manoti ..Baada ya kukataliwa pesa zake akaondoka kwa hasira na kurudi kwenye biashara zake.sijui baada ya hapo alikwenda kwenye chama gani hiyo atajijua mwenyewe..tarehe 25 ikafika uchaguzi ukafanyika ..matokeo yakatangazwa hatimae mgombea wa CCM akashinda na kuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania bwana Magufuli..
Baada ya kuapishwa Rais akaanza kazi mara moja na sera yake ilikuwa ni kuanza na kupambana na mambo makuu manne la kwanza ni Kuondoa umaskini kwa watu kufanya kazi,pili kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira hasa kwa vijana,tatu,Kuendeleza vita dhidi ya adui rushwa  na ubadhirifu wa mali ya umma na nne ni kuendeleza kudumisha amani,ulinzi na usalama ya maisha ya wananchi na mali zao..Baada ya rais kuanza kazi yake akaanza na fagia fagia la viongozi wabovu kwa kuwafukuza na kuwasimamisha kazi,Viongozi hao kumbe ndiyo walikuwa marafiki wakubwa na mfanyabiashara Manoti  ambao kumbe bwana manoti alikuwa akiwatumia kwenye kupitisha na kufanya mambo yake kinyume na utaratibu wa serikali na ndiyo maana bwana manoti alikuwa akipitisha mizigo anavyotaka..Balaa likazidi kumuandama bwana manoti pale aliposikia kuwa mabehewa yake yamezuiwa ili akayalipie kodi..alichanganyikiwa ikabidi afunge safari na kwenda, Manoti alipofika tu kwenye sehemu ya kulipia kodi akaanza kutoa pesa ili ayalipie akaambiwa hapana inabidi alipie mizigo yake yoote ya nyuma iliyokuwa inapita bila kulipiwa..ghafra akajikuta yupo sehemu mbaya kwake..Bwana Manoti akawa hana ujanja ikabidi alipe kodi zote anazodaiwa na sasa bwana manoti pesa yake inakwenda kihalali na hapo sasa hawezi kuwa na pesa nyingi kama alivyokuwa mwanzo.Maisha yakaanza kubadilika bwana Manoti akaanza kuuza vitu kidogo kidogo,biashara zake zikaanza kwenda kihalali akaacha tabia ya kumwaga pesa hovyo,pesa zikamuishia akabaki na pesa za halali za yeye na familia yake tu ..wale wapambe,taasisi,makundi ya kijamii aliyokuwa anawapa zile pesa haramu woote wakawa hawapewi tena pesa..Jamii yake iliyokuwa imemzunguka ikimtegemea yeye wakawa hohe hahe wameishiwa omba omba imekuwa na kikomo..bwana Manoti akaanza kuwaaminisha watu wake kuwa Rais amemchukulia pesa zake,kumbe ni uongo akuwaeleza ukweli watu wake kuwa pesa zote zile alizokuwa nazo mwanzo zilikuwa ni za wizi na alikuwa akiibia serikali..
Hadithi hii inatufundisha kuwa wale matajili waliokuwa wanamwaga mipesa ya vujo kwenye jamii sasa hakuna tena kitu hiko..badala ya kuwaambia watu ukweli wamekuwa wakishirikiana na vyama pinzani kuwadanganya watu kuwa Rais ameshikilia pesa zao na uchumi umeshuka..huu ni uongo tena ni uongo uliopitiliza Rais hajashika pesa za mtu.Waseme tu ukweli kuwa zile pesa za dili siku hizi hakuna tena.Na habari nilizozipata nasikia Yule mtoto wa mzee Manoti anyeitwa Nyamigawa ameshakuwa Chizi ukipita kwenye mataa ya pale fire utamuona.
Maskini Nyamigawa.


Posted by Ally Mtakuja
Mzalendo na mwenye uchungu na taifa  



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni