Alhamisi, 11 Septemba 2014

OMY DIMPOZ ALIVYOWAPAGAWISHA MABINTI WA MAMTONI


HII SASA NI KUFURU!!! P-SQUARE WAWEKA SOFA {SAMANI} ZA DHAHABU NDANI YA NYUMBA YAO MPYA....

‘We Talking Money You Talking Nonsense’ huenda ikawa kauli nzuri kuelezea hiki walichokifanya P-Square kwa sasa.


Hakuna ubishi kuwa, kwa hiki walichokifanya sasa, na kama macho yetu hayatudanganyi kwa hiki yanayokiona, mapacha hawa wamefanya kufuru. Kama hii inayoonekana ni dhahabu kweli, basi P-Square, hela wanayo.

Peter ameshare picha hizi nne ambazo wiki hii zitakuwa gumzo barani Afrika ambapo kwenye picha moja inayomuonesha pacha mwezie Paul akiwa amesimama kwenye sebule mpya inayoaminika kuwa ya nyumba yao mpya, ameandika ‘Goldenworld #blessed.’
Kwenye picha nyingine, wanaoonekana wakiwa pamoja kwenye sebule hiyo iliyotawaliwa na kile kinachoonekana kama dhahabu zilizozunguka sofa za kuvutia na Peter ameandika: #2kings…… Work hard,play harder.’Picha nyingine inamuonesha Peter akiwa peke yake kwenye meza ya chakula, kubwa, iliyojaa vyombo vya thamani vya kuvutia na ameandika: A king in my own world…. #Blessed.”

Hatimaye Serikali yabariki TANESCO kupandisha bei za umeme....Naibu waziri asema "atakayeshindwa kumudu gharama hizo, atumie kibatari..."

Naibu Waziri wa umeme, Mh George Simbachawene, amesema kwamba serikali imekubali TANESCO waongeze gharama za umeme kwa 68% kama walivyokuwa wameomba.


Simbachawene ameitoa kauli hiyo wakati akiongea katika kipindi cha Kumepambazuka kupitia Radio One leo asubuhi.



Amesema kwamba hata kama TANESCO wakiongeza gharama za umeme hadi kufikia Tsh 800 kwa unit bei hiyo ni nafuu kuliko gharama za kununua mafuta ya taa.

Mh Simbachawene ametahadharisha kwamba kama mtu ataona kwamba gharama za umeme ni kubwa, basi akawashe kibatari au akae gizani.

WABUNGE WATANYONGWA HADHARANI

BAADHI ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wamesema wala rushwa pamoja na wahujumu uchumi adhabu yao iwe ni kunyongwa. Wametaka Katiba mpya inayoenda kuandikwa itamke hivyo ili kufanya viongozi wa kisiasa kuogopa kama ilivyo kwenye nchi nyingine.

Sababu ya wajumbe hao kupendekeza jambo hilo ni kwamba uhujumu uchumi na rushwa nchini limekuwa tatizo kubwa kwa viongozi. Kutokana na ukiukwaji huo wa maadili, wamesema umefika wakati wa kuweka bayana suala hilo kwenye sheria mama.

Miongoni mwa waliochangia ni Paul Makonda aliyesema suala hilo likiwekwa bayana, litaokoa fedha nyingi za walipa kodi ambazo kwa sasa baadhi ya viongozi wanazichota na kwenda kuzihifadhi nje ya nchi.

Pia alipinga kuruhusu viongozi wa nchi kufungua akaunti nje ya nchi.

“Kwa nini viongozi hao washindwe kuhifadhi fedha zao ndani ya nchi, wanafanya biashara gani hadi wakafungue benki nje ya nchi? “Tusiruhusu jambo hili na napendekeza kwamba kiongozi atakayebainika amekula rushwa na kuhujumu uchumi huyo anyongwe,” alisema Makonda.

Yusuf Singo pia alisema maadili yanazidi kuporomoka kwa viongozi, jambo linalorudisha nchi nyuma.

Alitaka Katiba isisitize maadili kwa kada hiyo na ambao watakiuka wanyongwe. Alitoa mfano wa Japan kuwa kiongozi wa kisiasa anapochunguzwa kwa kujihusisha na rushwa anatoa machozi kwa sababu hajui hatima yake.

“Tunataka na sisi ifike wakati kiongozi akianza kuchunguzwa atoe machozi,” alisema. Dk Mary Mwanjelwa katika mchango wake alisema rushwa imekuwa adui mkubwa wa maendeleo ya Watanzania.

Alisema isipopingwa kuanzia kwenye Katiba, nchi itakuwa inajichora. Alisema Bunge halitaeleweka kama halitaweka jambo hilo kwenye Katiba, kwa sababu wananchi wengi wameteseka ndani ya nchi yao kwa sababu ya rushwa.

Alisema pia wapo viongozi wengi wasio na maadili na ndiyo maana wanajihusisha na vitendo vya rushwa.

Kwa upande wake, Profesa Mark Mwandosya alisema tatizo la rushwa haliwezi kutenganishwa na haki za binadamu kutokana na kukosesha wananchi maendeleo.

Profesa Mwandosya alisema Katiba lazima itambue adui wa haki za wananchi ni rushwa.

Alipendekeza suala hilo litambulike kikatiba na serikali zote mbili zitunge sheria kali za kupambana na rushwa kuhakikisha wananchi wanapata haki zao za msingi bila kutoa wala kupokea rushwa.

Naye Gerison Lwenge alisema Katiba itambue jambo hilo na ikemee vikali kwa wanaotoa na wale wanaopokea.

Alisema kwa ahli ilivyo, wanaobanwa zaidi ni wale ambao wanapokea na akapendekeza sheria kali zitungwe kubana pia wanaotoa.

Alishauri Kamisheni isimamie suala hilo la rushwa badala ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Kwa mujibu wa Lwenge, Kamisheni ni chombo kikubwa zaidi kuliko ilivyo kwa taasisi. Alisema kazi yake itakuwa ni kuzuia zaidi na si kutibu pekee.

Jesca Msambatavangu alisema Takukuru wanafanya kazi vizuri na walishindwa kupambana na rushwa kwa vile hawana uhuru wa kutosha.

Alisema kama Takukuru wakipewa meno kupitia Katiba mpya, watashughulika kwa uhuru zaidi katika kupambana na tatizo la rushwa nchini.

HIZI DAWA ZA KUONGEZA UCHUNGU KWA WAJAWAZITO ..KUMBE NI HATARI

MATUMIZI ya dawa za kienyeji kwa ajili ya kuongeza uchungu na kujifungua mapema, imeelezwa kuchangia zaidi vifo kwa wajawazito.

Mganga Mkuu wa Mkoa Kigoma, Dk Leonald Subi alisema hayo mjini Kigoma kwenye kikao cha wadau wa afya.

Kikao hicho kilihusisha kufanya tathmini na kuona hatua za kuchukua kukabiliana na vifo vya wajawazito na watoto wakati wa kujifungua mkoani humo.

Kiliitishwa na shirika la Wolrd Lung Foundation. Dk Subi alisema kuwa licha ya jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali kwa kushirikiana na wadau wengine, kukabiliana na hali hiyo, bado wajawazito wanajifungulia majumbani na kutumia dawa hizo hatarishi kwa maisha yao.

Alisema kumekuwa na upungufu wa vifo vya wajawazito na ongezeko la vifo vya watoto.

Alisema vifo vya wajawazito vimepungua kutoka vifo 74 mwaka 2009 hadi kufikia 49 kwa mwaka jana huku vifo vya watoto wachanga vikiongezeka kutoka 720 mwaka 2009 na kufikia 840 mwaka jana.

Mkurugenzi wa Miradi wa World Lung Foundation, Dk Nguke Mwakatundu alisema shirika lake linaboresha huduma za mama na mtoto mkoani humo, lakini changamoto ya vifo vya wajawazito ni kubwa, kutokana na kujifungulia majumbani.

Ijumaa, 25 Aprili 2014

PICHA ZA SAFARI YA DOTNATA ARUSHA














WIKI IJAYO TUTAENDELEA KUWALETEA MFULULIZO WA PICHA ZA DOTNATA ARUSHA

CHUCHU NA RAY KAMA KIM NA KANYE WEST






KUKOPI na kupesti bila kuboresha! Mastaa wenye mapenzi kama ya njiwa kutoka kiwanda cha filamu za Kibongo, Chuchu Hans na Vincent Kigosi ‘Ray The Greatest’ wamekuwa wakitupia swaga za picha kama zile za Kim Kardashian na mwandani wake, Kanye West.

Kupitia kurasa zao za mitandao ya kijamii, Chuchu na Ray ambao majina yao yameunganishwa na kuwa Chura wamekuwa wakichukua sampo za picha za akina Kim nao kujifotoa kisha kuzisambaza.



“He! Mmewaona Chuchu na Ray? Eti wanakopi na kupesti swaga kama zile za Kim na Kanye kisa mapenzi yamekolea,” alisema mdau mmoja baada ya kuziona picha hizo mtandaoni.

WEMA AFUNGUKA “NAJUTA KUMLIPIA KAJALA MIL 13″….


WEMA NA KAJALA














Akizungumza na Ijumaa katika exclusive interview Jumanne iliyopita, Wema ambaye pia ni staa mkubwa wa sinema za Kibongoalisema kuwa kuna mambo mazito ambayo yamesababisha yeye kuingia kwenye gogoro kubwa na Kajala.Wema au Beautiful Onyinye alisema kwamba mambo hayo ndiyo yamemsababishia maumivu ya moyo na kutokwa machozi kila wakati.

“Leo (anataja jina la mwandishi), ngoja nikuelezee kila kitu kinachohusiana na mimi na Kajala juu ya tofauti zetu.“Naamini baada ya kusimulia kisa na mkasa nitakuwa nimeutua huu mzigo mkubwa nilionao ndani ya moyo wangu.

“Baada ya hapo sitapenda tena kuzungumzia ishu inayonihusu mimi na Kajala,” alianza kufunguka Wema.

UZINDUZI WA KIGODORO
Katika maelezo yake, cha kwanza, Wema ni uzinduzi wa Filamu ya Kigodoro uliofanyika hivi karibuni kwenye Ukumbi wa Dar Live, Mbagala-Zakhem jijini Dar ambapo yeye alisema kuwa alianza kuyaamini yale yaliyokuwa yakisemwa na watu kuhusiana na Kajala.

Wema alisema kabla ya tukio, akiwa saluni akijiandaa kwa ajili ya uzinduzi huo, ghafla Kajala alimharibia ‘mudi’. “Unajua ile Saluni ya (anataja jina la saluni) pale Kinondoni, ina sehemu mbili, juu na chini, sasa mimi nilikuwa juu na Aunt (Ezekiel) tunatengeneza nywele.

“Niliposhuka kwa ajili ya kuosha nywele, nikamuona Kajala, kwa kuwa nilikuwa sijaonana naye siku nyingi na tayari maneno yalishaanza kuwa mimi na Kajala tuna bifu, nikaona nioneshe kuwa sina bifu naye.
“Kweli nilipiga makelele ya furaha nilivyomuona K, nikawa nakimbia kwenda kumkumbatia, kiukweli niliishiwa nguvu baada ya kunikwepa na kusema nooo…Wema usinikumbatie na kuanza kutoa maneno ya dharau eti nitamchafua.

“Kusema kweli niliishiwa nguvu na kuona kama vile kizunguzungu huku aibu ikinijaa ghafla kwani pale kulikuwa na watu wengi, basi huwezi kuamini, nilishindwa kujizuia nikajikuta namtukana, sikumbakisha.
“Wakati namtukana alikuwa amekaa kwenye kiti cha kuoshwa, nikaenda nikamsukuma na kumfukuza pale kwenye kiti ili nikae nioshwe, huwezi amini hali ya hewa iliharibika ghafla kwani sikuwa na mudi tena,” alitiririka Wema.

SAFARI YA ARUSHA KATIKA SHOO YA MIRROW
Wema alisema kuwa baada ya kutofautiana pale saluni, hakuwa na kinyongo, safari ya Arusha ilipofika walikwenda kumsapoti msanii wao wa Bongo Fleva anayesimamiwa na Kampuni ya Endles Fame Production.

Wakiwa njiani, kwa mujibu wa Wema, yeye alikuwa hana fedha taslimu za kutosha zaidi ya kubeba kadi zake saba za ATM tofauti hivyo alimwambia Kajala ampe shilingi laki tatu kwa ajili ya watu kula na kunywa njiani pamoja na matumizi madogomadogo.

Alisema Kajala hakuwa na shilingi laki tatu akampa shilingi laki mbili na elfu themanini.
Aliendelea kutoa ya moyoni: “Tulipofika Arusha Kajala alimwita ndugu yake mmoja anayeitwa Doli kisha akamwambia achukue fedha alizokuwa nazo akamuwekee benki kwa sababu sikuwa na fedha na nilianza kukopa eti nilijishaua kuandaa shoo nikitegemea fedha zake.

“Wakati K anazungumza hivyo kulikuwa na watu watatu, mimi sina hili wala lile nikamuuliza mtu mmoja mbona siwaoni, wamekwenda wapi?
“Ndipo nikafungukiwa kuwa wananikimbia kisa nimemkopa K hizo laki mbili na elfu themanini, kiukweli iliniuma sana, Kanalalamikia laki mbili? Tena hakunipa bali alinikopesha?

“Nilijiuliza amesahau mimi nilitoa Sh. milioni 13 kumlipia faini asiende jela miaka saba? Nguo nikinunua nanunua sare, nywele sare, viatu sare, mapochi sare, ninachokula na kunywa mimi ndicho hichohicho.
“Siku zote wakati akiwa gerezani nguo, viatu, hereni yaani kila kitu nilikuwa ni mimi, leo laki mbili na elfu themanini, niliyomuazima ananitangazia kwa watu (anataja jina la mwandishi)?

“Iliniuma sana basi palepale, nikaenda benki nikatoa Sh. milioni mbili, nikamlipa fedha zake, nikakaa kimya nikijifanya sijui chochote kinachoendelea kwani ningefanya chochote ningeharibu shoo na isingekuwa na maana yoyote ya sisi kwenda Arusha.”

WAREJEA DAR, MAANDALIZI YA FILAMU YAKE YAANZA
Wema alisema waliporejea Dar, alimwambia Kajala kuwa kuna mtu aliyekuwa amempa stori hivyo alimuomba wafanye filamu wawili.

Alisema kwamba Kajala alikubali na kusema kuwa atachangia Sh. milioni tano katika bajeti ya filamu hiyo.Baada ya kusikia hivyo, Wema alisema alifarijika, alipokwenda kumweleza ‘bebi’ wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, naye Diamond akasema atatoa Sh. milioni tano hivyo jumla itakuwa Sh. milioni kumi ikapita bajeti iliyokuwa imepangwa ya Sh.milioni nane.

Anaendelea: “Tukiwa katika maandalizi ya mwisho tuanze ku-shoot, K alinipigia simu akaniambia hawezi ku-shoot kwani alikuwa na safari ya kwenda China labda wa-shoot vipande vyake, nikamwambia basi aende akirudi tutatengeneza nyingine.

“Baada ya kuona hivyo ndipo nikamchukua Aunt tutengeneze filamu. K alipoona nimemchukua Aunt, akanipigia simu na kuanza kuongea shiti.“Nilijiuliza mbona mwenzangu amesahau ghafla wema wangu niliomtendea au kwa kuwa tangu aanze vijisafari vyake vya kwenda China anapata

WEMA AFUNGUKA “NAJUTA KUMLIPIA KAJALA MIL 13″….

WEMA NA KAJALA NJE YA MAHAKAMA

KAMA kuna kitu kinakukwaza ndani ya moyo wako, siku zote ukikaa nacho kitazidi kukuumiza lakini ukiamua kumtafuta mtu ambaye umeshibana naye na kumsimulia, moja kwa moja utakuwa umeutua mzigo!

Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ akiwa Kajala Masanja.

Hicho ndicho amekifanya Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ kwa kuweka kweupe chanzo cha ugomvi wake na staa mwenzake, Kajala Masanja huku akijuta kumlipia mwanadada huyo zile Sh. milioni 13 za faini ili asiende jela miaka saba.

Akizungumza na Ijumaa katika exclusive interview Jumanne iliyopita, Wema ambaye pia ni staa mkubwa wa sinema za Kibongoalisema kuwa kuna mambo mazito ambayo yamesababisha yeye kuingia kwenye gogoro kubwa na Kajala.Wema au Beautiful Onyinye alisema kwamba mambo hayo ndiyo yamemsababishia maumivu ya moyo na kutokwa machozi kila wakati.

“Leo (anataja jina la mwandishi), ngoja nikuelezee kila kitu kinachohusiana na mimi na Kajala juu ya tofauti zetu.“Naamini baada ya kusimulia kisa na mkasa nitakuwa nimeutua huu mzigo mkubwa nilionao ndani ya moyo wangu.

“Baada ya hapo sitapenda tena kuzungumzia ishu inayonihusu mimi na Kajala,” alianza kufunguka Wema.

UZINDUZI WA KIGODORO
Katika maelezo yake, cha kwanza, Wema ni uzinduzi wa Filamu ya Kigodoro uliofanyika hivi karibuni kwenye Ukumbi wa Dar Live, Mbagala-Zakhem jijini Dar ambapo yeye alisema kuwa alianza kuyaamini yale yaliyokuwa yakisemwa na watu kuhusiana na Kajala.

Wema alisema kabla ya tukio, akiwa saluni akijiandaa kwa ajili ya uzinduzi huo, ghafla Kajala alimharibia ‘mudi’. “Unajua ile Saluni ya (anataja jina la saluni) pale Kinondoni, ina sehemu mbili, juu na chini, sasa mimi nilikuwa juu na Aunt (Ezekiel) tunatengeneza nywele.







“Niliposhuka kwa ajili ya kuosha nywele, nikamuona Kajala, kwa kuwa nilikuwa sijaonana naye siku nyingi na tayari maneno yalishaanza kuwa mimi na Kajala tuna bifu, nikaona nioneshe kuwa sina bifu naye.
“Kweli nilipiga makelele ya furaha nilivyomuona K, nikawa nakimbia kwenda kumkumbatia, kiukweli niliishiwa nguvu baada ya kunikwepa na kusema nooo…Wema usinikumbatie na kuanza kutoa maneno ya dharau eti nitamchafua.

“Kusema kweli niliishiwa nguvu na kuona kama vile kizunguzungu huku aibu ikinijaa ghafla kwani pale kulikuwa na watu wengi, basi huwezi kuamini, nilishindwa kujizuia nikajikuta namtukana, sikumbakisha.
“Wakati namtukana alikuwa amekaa kwenye kiti cha kuoshwa, nikaenda nikamsukuma na kumfukuza pale kwenye kiti ili nikae nioshwe, huwezi amini hali ya hewa iliharibika ghafla kwani sikuwa na mudi tena,” alitiririka Wema.

SAFARI YA ARUSHA KATIKA SHOO YA MIRROW
Wema alisema kuwa baada ya kutofautiana pale saluni, hakuwa na kinyongo, safari ya Arusha ilipofika walikwenda kumsapoti msanii wao wa Bongo Fleva anayesimamiwa na Kampuni ya Endles Fame Production.

Wakiwa njiani, kwa mujibu wa Wema, yeye alikuwa hana fedha taslimu za kutosha zaidi ya kubeba kadi zake saba za ATM tofauti hivyo alimwambia Kajala ampe shilingi laki tatu kwa ajili ya watu kula na kunywa njiani pamoja na matumizi madogomadogo.

Alisema Kajala hakuwa na shilingi laki tatu akampa shilingi laki mbili na elfu themanini.
Aliendelea kutoa ya moyoni: “Tulipofika Arusha Kajala alimwita ndugu yake mmoja anayeitwa Doli kisha akamwambia achukue fedha alizokuwa nazo akamuwekee benki kwa sababu sikuwa na fedha na nilianza kukopa eti nilijishaua kuandaa shoo nikitegemea fedha zake.

“Wakati K anazungumza hivyo kulikuwa na watu watatu, mimi sina hili wala lile nikamuuliza mtu mmoja mbona siwaoni, wamekwenda wapi?
“Ndipo nikafungukiwa kuwa wananikimbia kisa nimemkopa K hizo laki mbili na elfu themanini, kiukweli iliniuma sana, Kanalalamikia laki mbili? Tena hakunipa bali alinikopesha?

“Nilijiuliza amesahau mimi nilitoa Sh. milioni 13 kumlipia faini asiende jela miaka saba? Nguo nikinunua nanunua sare, nywele sare, viatu sare, mapochi sare, ninachokula na kunywa mimi ndicho hichohicho.
“Siku zote wakati akiwa gerezani nguo, viatu, hereni yaani kila kitu nilikuwa ni mimi, leo laki mbili na elfu themanini, niliyomuazima ananitangazia kwa watu (anataja jina la mwandishi)?

“Iliniuma sana basi palepale, nikaenda benki nikatoa Sh. milioni mbili, nikamlipa fedha zake, nikakaa kimya nikijifanya sijui chochote kinachoendelea kwani ningefanya chochote ningeharibu shoo na isingekuwa na maana yoyote ya sisi kwenda Arusha.”

WAREJEA DAR, MAANDALIZI YA FILAMU YAKE YAANZA
Wema alisema waliporejea Dar, alimwambia Kajala kuwa kuna mtu aliyekuwa amempa stori hivyo alimuomba wafanye filamu wawili.

Alisema kwamba Kajala alikubali na kusema kuwa atachangia Sh. milioni tano katika bajeti ya filamu hiyo.Baada ya kusikia hivyo, Wema alisema alifarijika, alipokwenda kumweleza ‘bebi’ wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, naye Diamond akasema atatoa Sh. milioni tano hivyo jumla itakuwa Sh. milioni kumi ikapita bajeti iliyokuwa imepangwa ya Sh.milioni nane.

Anaendelea: “Tukiwa katika maandalizi ya mwisho tuanze ku-shoot, K alinipigia simu akaniambia hawezi ku-shoot kwani alikuwa na safari ya kwenda China labda wa-shoot vipande vyake, nikamwambia basi aende akirudi tutatengeneza nyingine.

“Baada ya kuona hivyo ndipo nikamchukua Aunt tutengeneze filamu. K alipoona nimemchukua Aunt, akanipigia simu na kuanza kuongea shiti.“Nilijiuliza mbona mwenzangu amesahau ghafla wema wangu niliomtendea au kwa kuwa tangu aanze vijisafari vyake vya kwenda China anapata




Mtoto wa KAJALA akerwa na Ugomvi kati ya KAJALA na WEMA

KAJALA NA MWANAE


Kutokana na ugomvi unaoendelea kati ya Wema Sepetu na Kajala Masanja,mtoto wa Kajala aitwaye Paulette amesema anaumizwa na ugomvi huo na kwamba amekuwa akimtumia ujumbe Wema kumweleza anavyompenda.

Paulette alikuwa akizungumza na ‘Movie Leo’ ya kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM.


“Vimekuwa vinaniuma sana ila hata kama wakisema vitu vyote ataendelea kuwa mama yangu,” alisema.“Mimi naona mama yangu hana makosa yoyote wanavyomtukana,mimi nakuaga najisikia sana vibaya.


“Namwambia (Wema) mama yangu hata kama amekosea kitu chochote amsamehe kwasababu mimi nampenda Wema kama aunt yangu na ninampenda mama yangu tena sipendi nikiona wanatukanana wala nini napenda wawe marafiki,nataka nimwambie Wema nampenda sana,” alisema. Paula.

Jumatatu, 3 Februari 2014

ALLY MTAKUJA KUGOMBEA UDIWANI MWAKA 2015

vijana sasa wameamka baada ya kuona kuwa maeneo yao wanayoishi kukosa maendeleo.Hii ni kauri iliyotolewa na muheshimiwa mbunge jina kapuni baada ya kuisikia kauri ya kijana mpenda maendeleo ALLY MTAKUJA baada ya kutangaza nia yake ya kugombea udiwani kwenye kata ya tabata kwa kile kinachodaiwa kuwa kata hiyo imekosa kabisa maendeleo kwa kipindi cha miaka 10 mpaka sasa.Ilikuwa juzi kwenye kikao kilichohusisha wananchi wa tawi la tabata msimbazi magharibi katika kujadili maendeleo hususani barabara zilizofungwa kwa makusudi na watu wachache..Ally mtakuja alisimama na kuchangia hoja ambapo alitoa lawama zake kwa viongozi wa maeneo hayo kuonekana wamelala usingizi ndiyo maana eneo hilo lipo nyuma kimaendeleo hata hivyo baada ya kuchangia hoja Ally alimaliza kwa kuwaambia wananchi kuwa mwaka 2015 wampe kura za ndiyo kwani ameamua kujitoa kimaso maso kugombea udiwani wa eneo hilo jambo lililosababisha wananchi wote kulipuka kwa shangwe kubwa na kumshangilia huku wakiimba ,,diwani,,diwani,,diwani


hata hivyo mpaka sasa ALLY MTAKUJA amekataa kuweka wazi kuwa atagombea udiwani kwa tiketi ya chama gani .....hapana bado kuweka wazi ni mapema mno muda rasmi bado ila utakapofika kila kitu kitakuwa wazi...tupo kwa ajili ya kuleta maendeleo "alisema Ally
ALLY MTAKUJA AKIWA NA MSANII MAARUFU WA BONGO MOVIE AMANDA POSH KWENYE MOJA YA KAZI ZAKE





Alhamisi, 30 Januari 2014

JAPHET KASEBA ANABADIRIKA KAMA KINYONGA

Bingwa wa kickboxing anayetambulika ulimwengu mzima bwana JAPHET KASEBA au kama wengi walivyozoea kumwita CHAMPION ameendelea kuungurumisha kipaji chake kengine cha sanaa ya uigizaji kwa kasi kubwa.Baada ya kushiriki kwa mara nyengine tena kwenye filamu ya DOTNATA inayojulikana kwa jina la JANI CHANGA..Japhet ambaye ameshiriki kwenye filamu hiyo kama mfanyabiashara mkubwa wa madini ameonesha uwezo mkubwa kwenye sehemu hiyo tofauti na vile watu walivyomzoea..Akiongea kwa niaba ya mume wake dada PENDO KASEBA ambaye pia hata yeye ni mshiriki wa filamu hiyo alisema.....watu wamezoea kumuona KASEBA kwenye mapigano tu...ukwelli ni kwamba Kaseba wa sasa hivi ukiachilia mbali fani yake ya kickboxing lakini pia ni msanii mzuri sana kwenye tasnia ya uigizaji na ameonesha kumudu kila sekta anayopangwa...Alipoulizwa ushiriki wake anajisikiaje kwenye sehemu hiyo ya mfanyabiashara wa madini na siyo ule upande aliouzoea yeye wa ngumi.Bwana KASEBA alisema "Unajua mimi ni bingwa wa kickboxing,lakini pia ni msanii wa uigizaji,sasa unapokuwa msanii huwezi kuchagua mfumo mmoja wa uigizaji wako inakupasa uwe unabadilika badilika ili kuwapa burudani wapenzi wako...Kwa hiyo nilivyoambiwa na mama DOTNATA kuwa safari hii natakiwa nicheze kama mfanyabiashara wa madini wala sikukataa nilifurahi na nimecheza kwa moyo wangu wote nafikiri hata madirector wangu watakuwa mashahidi kwa hilo"DOTNATA ENTARTAINMENT inakuja na filamu mpya ambayo mpaka sasa imeshamaliza kushutiwa na sasa ipo studio kwa ajili ya editing..
CHAMPION JAPHET KASEBA

Jumapili, 12 Januari 2014

Hawa ndo wachezaji pekee aliokua akiwahofia ubingwa Yaya Toure

pengine kulingana na viwango sawa vya uchezaji au wao kukuzidi maarifa kidogo,hiko ndicho kilichotokea kwa Nyota toka Manchester City mchezaji Yaya Toure ambaye ameshinda kwa mara ya tatu mfululizo tuzo ya mchezaji bora barani Afrika,ushindi ambao umekosolewa na maafisa wakuu wa soka nchini Nigeria.

Toure mwenye umri wa miaka 31 ambaye ni raia wa Cote d’Ivoire alishinda pia tuzo ya Shirikisho la Soka barani Afrika – CAF, mwaka wa 2011 na 2012 huku John Obi Mikel wa Nigeria ambaye anachezea klabu ya Chelsea ya Uingereza akichukua pili na nafasi ya tatu ikishikwa na Didier Drogba kutoka huko huko Cote d’Ivoire.

Hiki ndicho alichokizungumza Toure baada ya kutangazwa mshindi ‘Kwa kweli ilikuwa vigumu sana kushinda,kwa sababu kulikuwa na wapinzani wakali mbele yangu Obi Mikel na Didier Drogba kwa hivyo nilidhani nitashindwa na sasa nimebahatika na nina furaha kwa mafanikio yangu Ninapenda kile ninachofanya’

Muda mfupi baada ya kutangazwa ushindi huo wa Toure Maafisa wakuu wa soka nchini Nigeria waliukosoa utaratibu uliotumiwa kumpata mshindi,Utaratibu uliotumika ni wa Makocha wa timu 54 za mataifa wanachama wa CAF huwapigia kura wachezaji 10 wanaoteuliwa kwa mizani ya pointi moja hadi kumi, huku atakayepata pointi nyingi ndiye anayeondoka na tuzo hiyo.

Toure alikusanya jumla ya pointi 373 na akapigiwa kura na makocha 28 na kumpa mchezaji huyo wa Manchester City ya Uingereza ushindi wa tatu mfululizo baada ya kunyakua taji hilo mwaka wa 2011 na 2013 huku Kiungo wa Chelsea Mikel, akiwa pili na jumla ya pointi 275.


mchezaji bora wa afrika yaya toure

DUH ! EMBU MSIKILIZE JACKY WOLPER...HUU NDIYO UBONGO MOVIE AU ? KAWEKA WAZI KUHUSU KUTEMBEA NA ...ALI KIBA.....JUX....NA DIAMOND


SUKARI YA WAREMBO DIAMOND PLATNUM

Muingizaji wa filamu nchini,Jacklyn Wolper amesema pamoja na kuwa na mahusiano na wasanii wenzake akiwemo Diamond,Jux. lakini Ally Kiba ndiye msanii pekee aliyemtambulisha kwenye ulimwengue wa mtamu wa mapenzi.

Akiongea na Global Publishers,muingizaji huyo alisema aliachana na Ally Kiba kwasababu ya wanawake wengi walikuwa wakimtamani kimapenzi.


WOLPER
' “Ni kitambo kidogo. Wote hatukuwa mastaa lakini yeye alifanikiwa kuchomoka. Kabla ya Ali (Kiba) nilikuwa na mwanaume lakini hatukuduu kwa maana ya utu uzima, ilikuwa yale ya kitoto. Lakini Ali ndiye hasa aliyeniingiza kwenye ulimwengu wa mapenzi'Alisema Wolper


“Ali akawa staa. Alipokwenda nje nikasikia wanawake wanamshobokea. Sasa mimi sikutaka karaha nikakaa pembeni lakini jamaa ni mtu poa sana na tukikutana tunasalimiana freshi kabisa.”alisema Wolper
ALI KIBA
Vipi kuhusu Jux?
“Jux (msanii wa Bongo Fleva, Juma Khalid) nilikuwa naye kabla ya Dallas na yule
mwanaume wangu niliyeachana naye wakati wa Dallas. Katika maisha yangu nilimpenda sana Jux. Siyo marioo ni mwanaume mtafutaji aliyejiamini. Kwa sasa sipo naye. Dallas pia alichangia mimi kuachana na Jux,”alisema.



“Ni kweli niliwahi kuwa na Diamond (msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul). Tulikuwa na uhusiano lakini pia alikuwa mshirika wa kibiashara (hataki kuitaja). Yeye alikuwa hawezi kulala bila kuniona, lakini tulikaa kama mwezi mmoja, kwa sasa amebaki kuwa rafiki yangu na siyo mpenzi tena kama zamani,” alisema Wolper.